Leviticus 24:1-6

Mafuta Na Mikate Mbele Za Bwana

1 Bwana akamwambia Musa, 2 a“Waagize Waisraeli wakuletee mafuta safi ya zeituni yaliyokamuliwa kwa ajili ya mwanga ili taa ziwe zinawaka daima. 3 bNje ya pazia la Ushuhuda ndani ya Hema la Kukutania, Haruni ataziwasha taa mbele za Bwana kuanzia jioni hadi asubuhi bila kuzima. Hili litakuwa agizo la kudumu kwa vizazi vijavyo. 4 cTaa zilizo juu ya kinara cha dhahabu safi mbele za Bwana lazima zihudumiwe daima.

5 d“Chukua unga laini, uoke mikate kumi na miwili, ukitumia sehemu mbili za kumi za efa
Sehemu mbili za kumi za efa ni sawa na kilo mbili.
za unga kwa kila mkate.
6 fIweke katika mistari miwili, kila mstari mikate sita, uiweke mbele za Bwana juu ya meza iliyotengenezwa kwa dhahabu safi.
Copyright information for SwhKC